Maandalizi; dakika 10
Muda wa kupika; dakika 10
Muda jumla; dakika 20
Mahitaji
Kwa wali na mbogamboja
Vikombe 2 wali uliopikwa
Vijiko 2 vya chakula mafuta ya kupikia
Kijiko 1 cha chai kitunguu saumu
Kitunguu maji 1 cha wastani
Karoti 1
Kikombe 1 maharagwe machanga
Kitunguu cha majani
Kwa sosi
Vijiko 2 vya chakula sosi ya soya
Kijiko 1 cha chakula mafuta ya ufuza (Ukipenda)
Kijiko 1 cha chai tangawizi (ukipenda)
Mbegu za ufuta (ukipenda)
Maelekezo
Andaa viungo; katakata maharagwe, karoti, majani ya kitunguu na kitunguu maji vipande vidogovidogo sana; Twanga kitunguu saumu na tangawizi, weka pembeni
Kwenye kikaangio kikubwa katika moto wa juu kiasi, chemsha mafuta. Ongeza kitunguu saumu mpaka kiive, halafu uongeze kitunguu maji. Pika mpaka kiive
Ongeza karoti na maharagwe machanga. Pika mpaka viive kama utakavyopenda wewe
Ongeza wali changanya vizuri
Changanya sosi ya soya, mafuta ya ufuta na tangawizi kwenye bakuli, weka pembeni. Ongeza mchanganyiko wa sosi na kitunguu cha maji. Pika kwa dakika nyingine 1, ipua
Pakua cha moto
Nyunyizia mbegu za ufuta kwa juu ukipenda
Napenda Sana hiki chakula,kitamu mno,, ila sijawah pika mwenyewe,,, ila nitajaribu,,, Ahsante dada
Rahisi sana kupika, unahitaji dakika 20 tu maandalizi na kupika. Good luck;)
Asante sana nilikuwa nikiona tu sasa nitajifunza kwa kumpikia mpenz wngu siku yake ya kuzaliwa
Ataenjoy sana, good luck and enjoy
Sijafahamu sosi unaipika kisha unamwagia au unaweka ktk mchanganyiko wa wali?
Unaichanganya na wali
thanks kwa mafunzo
maana napenda sana kupika nadhani,,mafunzo yako yatanifaa
Enjoy dear
I will try this weekend, thanx luv
Good luck dear;)
Dada Jane unatusaidia wengi napenda kubadilisha pishi…ila siunaweza pika zaidi ya vikombe vili vya mchele? Swali lingine mchele tuna chemsha tu ?
Wali pika kiasi unachotaka wewe, zidisha viungo vingine vyote au kadiria kiasi utakachoona kinatosha. Mchele unapika kama wali wa kawaida, mimi nimetumia kiporo cha wali wa kawaida tu wa kuchemsha na maji, mafuta na chumvi. Unaweza pia kuongeza au kupunguza viungo vingine ambavyo unapendelea wewe
Jane hongera sana kwa kweli I am so amazed by your work
Thank you dear, enjoy;)
Nmejaribu sikujuaga kama naweza tumia soy sauce kwenye wali i was really amazed kilivyoturn out to be waaay delicious, thanks Jane
Am happy umeufurahia my dear, enjoy:)
Dada jane nakupenda utanifanya niwe mwanamke mpambanaji natalajia kua mama ntilie napenda kupika ila sikua najua nitaandaaje chakula viungo kiungo gani nitaweka ilinipate chakula kizur lengo langu naimani litatimia nakupenda dada jane