Photo credit; Laissa Miller
Maandalizi; dakika 20
Muda wa kupika; dakika 15
Muda jumla; dakika 35
Mahitaji
Mayai 8 makubwa au 10 madogo
500g/ nusu kilo nyama ya kusaga
Kitunguu 1 cha wastani
Kijiko 1 cha chakula kitunguu saumu na tangawizi
Kijiko 1 cha chai bizari ya manjano
½ kijiko cha chai cayenne pepper
Kijiko 1 cha chai garam masala powder
¼ kikombe majani ya kotimiri/ giligilani
Chumvi kwa kuonja
½ kikombe unga wa mchele
Mafuta ya kukaangia
Maelekezo
Kwenye sufuria ya wastani katika moto wa juu kiasi, chemsha mayai yaive kama unavyopenda. Wakati mayai yanachemka, andaa viungo vingine; katakata majani ya kotimiri na kitunguu vipande vodogovidogo sana
Katika bakuli kubwa; weka nyama, kitunguu, majani ya kotimiri, kitunguu saumu na tangawizi, bizari ya manjano, pilipili ya unga na garam masala. Vunja yai moja uongeze kwenye mchanganyiko. Changanya vizuri, weka na chumvi kwa kuonja
Gawanya mchanganyiko kwenye madonge 6 hadi 8 yaliyolingana (inategemea na ukubwa wa mayai). Menya na mayai, weka pembeni
Funika kila yai na donge moja ya nyama. Hakikisha yai linakuwa katikati na limefunikwa vizuri na nyama. Sawazisha vizuri kwa juu kisha paka unga wa mchele kwenye madonge ya nyama kwa juu, hakikisha kila sehemu imefunikwa vizuri
Chemsha mafuta kwenye kikaangio katika moto wa wastani. Wakati mafuta yanachemka, piga yai moja lililobakia. Chovya kila egg chop kwenye yai, tingisha kidogo ili yai lililozidi litoke kabla ya kuweka kwenye mafuta
Kaanga mpaka ziwe na rangi ya kahawia
Hamishia egg chops zilizoiva kwenye sahani iliyowekwa tissues za jikoni au chujio la bati ili mafuta yote yachuje
Pakua kama utakavyopenda
Enjoy
Hello iv badala ya kuweka unga wa mchele unaweza weka wa ngano au?
Ndio, unaweza tumia unga wa ngano pia
Sijutii kukufollow mpnz. Naomba kuuliza hzo nyama za kusaga huichemshi hata kidogo. Na hilo yai bichi unachanganya kwenye nyama ee. Me nlikua najuaga hilo donge la nje ni mkate uliokandwa unachanganywa na nyama ya kusaga au samaki.
kwa recipe hii huitaji mkate, ni nyama mbichi isiyochemshwa, ukiichemsha itasambaratika haitashikana, itaiva kwenye kukaanga. Na yai bichi unachanganya kwenye nyama ili ishikane vizuri, unachanganya na viungo vingine kama maelekezo
Nilitaka kuuliza hili la kuvurugika ila nimepata jibu tayari…Thanks Jane
Good luck dear
Awwwew tamu saana nimejaribu 😘ubarikiwe saana
Thanks kwa feedback, nimefurahi sana umezipenda;)…ubarikiwe pia my dear
Mi nimeoka instead na imetoka mwake tu
Nice, am happy umezipenda and thanks kwa tip, nitajaribu kuoka na mimi next time;)
Duuh da jane I love you so much… ubarikiwe sana kwa kweli tunajifunza mengi kupitia page yako
Ahsante sana my dear, ninafurahi kujua mnajifunza chochote, barikiwa sana pia;)
Umeoka kwa muda gani?
Please angalia recipe vizuri, hazijaokwa zimekaangwa
👍👍👍👍, thanks màm, I love what you do
Thank you my dear;)
One of my Favorite food. Asante mama mudhungu. Love love love😘😘😍😍😍
Enjoy my dear
Ubarikiwe sana dada Jane ni kitu ambacho nilikuwa natamani sana nijue jinsi ya kutengeneza
Karibu my dear, good luck kwenye kutengeneza
Ubarikiwe Sana nimeona leo page yako Yan ubarikiwe mno
Ashante my dear, ubarikiwe sana pia